Jumatano, 13 Mei 2015

CHUO CHA UALIMU KOROGWE [KOCET]

Chuo cha Ualimu Korogwe [KOCET]
Chuo hiki kipo kilomita chache kutoka stendi kuu ya mabasi wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga. Chuo kwenye miaka ya 1990 hadi 19993 kilikuwa kinatoa mafunzo ya ualimu wa ngazi ya Diploma na cheti daraja A.
Pia kulikuwa kinatoa mafunzo kwa walimu waliokuwa wakibadili madaraja ya ualimu Daraja C kwenda A wakiitwa in-service.
Nilibahatika kusoma ualimu daraja la Diploma miaka mitatu na nilihitimu mwaka 1993.

Ninawakumbuka sana walimu wangu akiwemo mkuu wa chuo Mwl. Sylivester Mgoma, makamu mkuu wa chuo Mwl. Masawe, mwadili wa wanachuo Mwl. Gahu [RIP], Mwl. Mtoahanje, Mwl. Alex kocha wa mpira, Mwl. Muyombo, Mwl. Kipesha, Mwl. Mjema....
Lakini kulikuwa na watu maarufu kama mpishi mmoja akiitwa mgosi Hassani...
Hakika maisha ya KOCET yalikuwa matamusana. Nitatupiamo baadhi ya picha za KOCET miaka hiyoo.
 Picha ya muonekano kama unaingia chuoni

 Mitaa ya jengo la utawala miaka ya 1990 

Maoni 0:

Chapisha Maoni

Jisajili kwenye Chapisha Maoni [Atom]

<< Nyumbani