Jumatano, 13 Mei 2015

Jambo KOCET.....



Wapendwa wana KOCET!
Nina furaha kuwafahamisha kuwa nimeanzisha blog ambayo ninaamini pamoja na habari nyingine lakini pia itajikita sana katika kujadili mambo ya kijamii kwa manufaa yetu kwa ujumla.

Nimeanza na post hii yenye picha na habari za Chuo cha ualimu Korogwe ama tulikiita KOCET.

Chuo cha ualimu Korogwe kipo wilaya Korogwe kilomita chache kutoka stendi kuu ya mabasi ya Korogwe. Chuo hicho miaka ya 1990 hadi 1993 kilikuwa kikitoa mafunzo kwa walimu wa Diploma ya ualimu na daraja A.

Miye nilikuwepo chuoni hapo miaka ya 1990 hadi 1993 nilipomaliza Diploma yangu ya ualimu.

Tumekuwa tukijadiliana sana katika mitandao ya whatsapp na facebook, ni imani yangu hapa pia tutajadili na kufanya mambo makubwa kwa kadri tutakavyojaaliwa. Kupitia blog hii tutawapongezana kwa tuyuu, harusi, vyeo, elimu nk lakini pia tutapata habari nyinginezo zinazofanana na hizo.. 

Lakini pia tutajadili mambo ya kijamii, kiuchumi, saikolojia na mengineyo ambayo sisi tuna uzoefu nayo. Nachelea kujadili mambo ya kisiasa kwa sababu ya tofauti za kisiasa, mitizamo na kiitikadi nk.

Karibuni sana.....

Maoni 0:

Chapisha Maoni

Jisajili kwenye Chapisha Maoni [Atom]

<< Nyumbani